Friday, 5 September 2025

Muislam wa kwanza kuichezea England baada ya zaidi miaka 150


Djed Spence anatarajia kuwa chanzo cha hamasa kwa vizazi vijavyo ikiwa atakuwa mchezaji wa kwanza wa Kiislamu kuichezea timu ya taifa ya wanaume wa England.

Mchezaji huyo wa Tottenham anayecheza upande wa kushoto, ambaye tayari ameshacheza michezo sita kwa timu ya vijana ya England chini ya miaka 21, amejukmuishwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya wakubwa kwa mara ya kwanza kwa mechi za kufuzu kombe la Dunia dhidi ya Andorra na Serbia.

Hii ni hatua kubwa ya mageuzi kwa Spence, ambaye ni mchezaji wa zamani wa Middlesbrough, aliyetolewa kwa mkopo mara tatu na timu yake ya Spurs, kwenda Rennes, Leeds na Genoa, kabla ya kufanikiwa kuwa kwenye kikosi cha kwanza msimu uliopita.

Ingawa chama cha mpira wa miguu la England (FA), halifungamani na masuala ya dini ya mchezaji, inaelezwa kuwa Spence anakuwa mchezaji wa kwanza wa Kiislamu kuichezea timu ya taifa ya England.




Wednesday, 5 February 2025

Mfahamu Mo Salah "WA MCHONGO" anayetikisa mitandaoni


Ahmad Bahaa anafanana sana na mshambualiaji wa Liverpool na Misri Mohamed salah, na ameigiza katika matangazo mbalimbali ya televisheni.

Mhandishi Bahaa amesema katika kipindi cha runinga ya Al-Nahar TV kuwa ameshafanya matangazo ya simu na vinywaji laini akiwa ni mhusika kama Mo Salah pamoja na kampeni za kuacha madawa ya kulevya.
''Nimefanya matangazo mengi na Salah", alisema Ahmed Bahaa.
katika matangazo aliyofanya Bahaa anaonekana akiwa katika picha za mbali na sio za ukaribu sana na kuonesha sura.


Haki miliki ya pichaAL-NAHAR TV
Image captionJe unaona mapacha? hapo ni Mo Salah na Ahmad Bahaa

''Salah kwa kweli hawezi kukaa na kufanya tangazo moja kwa muda mrefu,'' Bahaa alielezea.
''Ninachukua muda mwingi kurekodi matangazo hapa na nitaenda pia Uingereza kumalizia kurekodi naye Salah, hii ni kuharakisha mambo kwa sababu yeye hana muda mwingi wa kufanya matangazo''
Taarifa hii iliwashtua sana watu katika mitandao ya kijamii, baadhi walitumiana video inayomuonesha Bahaa katika mtandao wa Twitter.
Shabiki mmoja alishangazwa na kudhani kuwa huenda Bahaa hucheza katika michuano ya Misri akishiriki kama Mo Salah.
''Yeye ni mtu mwenye mambo mengi na Misri kila siku inafungwa huenda huyu ndo anacheza na sio Mo Salah''
Misri alikua mwenyeji wa mashindano ya Kombe la Afrika lakini ilishindwa kufika Robo fainali.
Chanzo:BBC

KISA ASTON VILLA RASHFORD KUPOTEZA DILI LAKE NA NIKE



Rashford anaweza kupoteza kama 100% ya pesa za udhamini anazopokea kutoka kwa Nike kwasababu kampuni hiyo kubwa ya mavazi ya michezo inaichukulia Aston Villa kama kitengo cha chini cha klabu kuliko United . Nike pia inaweza kumuomba alipe kiasi cha ada za kusaini. (Mail Plus -Subscription required)


RAHSFORD : ASTON VILLA KWANZA KATIKA UHAMISHO WAKE



Mshambulizi wa Manchester United na Uingereza Marcus Rashford, 27, alikataa kuhamia klabu moja ya Uturuki kabla ya kujiunga na Aston Villa kwa mkopo. (Manchester Evening News )

MAKINDA HAWA WA MAN U KUPIGWA BEI



Manchester United bado iko tayari kumuuza winga wa Argentina Alejandro Garnacho, 20, na kiungo wa kati wa Uingereza Kobbie Mainoo, 19, msimu wa kiangazi (Guardian)


ALICHOKISEMA FADLU , SIMBA IKIIVAA FONTAIN GATE

 


KOCHA Mkuu wa Simba, Fadlu Davids, ameonekana kukoshwa na idadi kubwa ya mashabiki wa soka wanaojitokeza mikoani, akisema imekuwa chachu ya wachezaji wake kucheza kwa kujituma na kupata ushindi kwa asilimia 100 kwenye michezo ya ugenini ya Ligi Kuu Tanzania Bara ambayo imekuwa kama ipo nyumbani.

Akizungumza jijini Dodoma , ambako timu hiyo imeweka kambi ya muda kabla ya kuivaa Fountain Gate, katika mechi ya raundi ya 17 ya Ligi Kuu itakayopigwa kesho, Uwanja wa Tanzanite Kwaraa uliopo Babati mkoani Manyara, kocha huyo alisema ameshangazwa na idadi kubwa ya mashabiki wanavyojitokeza kwenye viwanja vya mikoani, na cha ajabu zaidi ni kwamba zaidi ya asilimia 90 wamekuwa wakiishangilia Simba kwa nguvu zote, kitu ambacho kinamfanya yeye na wachezaji wake kufanya kila juhudi kuhakikisha wanaondoka uwanjani na furaha baada ya mchezo.

"Nimeona kwenye michezo mingi mikoani, kumekuwa na mashabiki wengi uwanjani na wanakuwa wanatushangilia sisi, kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mashabiki walitia fora, walijitokeza kwa wingi zaidi, uwanja ulijaa sana, na karibuni wote walikuwa upande wetu, utagundua hilo bao linapofungwa, uwanja mzima unasimama kushangilia, tulikuwa ugenini, lakini ni kama nyumbani tu, hili pamoja na mambo mengine ya ufundi na mifumo, lakini nalo kiasi kikubwa linatusukuma sana kupata ushindi," alisema.

Simba imeshinda mechi zote nane ilizocheza ugenini mpaka sasa, ikiwa kinara wa kushinda mechi nyingi za ugenini mpaka sasa.

SOURCE: IPP

Monday, 19 August 2024

Mbappe ainunua Klabu yake iliyomkuza



 Kylian Mbappé amenunua hisa nyingi katika klabu ya Caen ambayo inashiriki Ligue 2 ya Ufaransa kwa takriban €20 milioni.

Akiwa na umri wa miaka 25, Mbappé anakuwa mmiliki mdogo zaidi wa klabu katika soka la Ulaya. Ununuzi huu unafuatia uhamisho wake wa hali ya juu kwenda Real Madrid, ambapo anaagiza mshahara mkubwa na mikataba ya kuidhinisha.

Akiwa na Caen, Mbappé anakusudia kubadilisha bahati ya kilabu,uwezekano wa kutengeneza njia kwa ajili ya jukumu la uwanjani siku zijazo.