Djed Spence anatarajia kuwa chanzo cha hamasa kwa vizazi vijavyo ikiwa atakuwa mchezaji wa kwanza wa Kiislamu kuichezea timu ya taifa ya wanaume wa England.
Mchezaji huyo wa Tottenham anayecheza upande wa kushoto, ambaye tayari ameshacheza michezo sita kwa timu ya vijana ya England chini ya miaka 21, amejukmuishwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya wakubwa kwa mara ya kwanza kwa mechi za kufuzu kombe la Dunia dhidi ya Andorra na Serbia.
Hii ni hatua kubwa ya mageuzi kwa Spence, ambaye ni mchezaji wa zamani wa Middlesbrough, aliyetolewa kwa mkopo mara tatu na timu yake ya Spurs, kwenda Rennes, Leeds na Genoa, kabla ya kufanikiwa kuwa kwenye kikosi cha kwanza msimu uliopita.
Ingawa chama cha mpira wa miguu la England (FA), halifungamani na masuala ya dini ya mchezaji, inaelezwa kuwa Spence anakuwa mchezaji wa kwanza wa Kiislamu kuichezea timu ya taifa ya England.







